C E O OF BMG

Picha yangu
FOUNDER AND OWNER OF BLACK GENERATION MEDIA GROUP, JORNALIST AND BROADCASTER BY PROFESIONAL.

Alhamisi, 28 Aprili 2016

RAIS JOHN MAGUFULI AMETENGUA UTEUZI WA MKURUGENZI MTENDAJI WA KITUO CHA UWEKEZAJI [TIC] JULIET KAIRUKI

Raisi wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania muheshimiwa John pombe Magufuli  ametengua  uteuzi wa mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha Uwekezaji  [TIC] juliet  kairuki , uteuzi  wake umetenguliwa kwa sababu ya kutochukua mshahara wake  tangu mwaka 2013, kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na katibu mkuu wa Biashara na uwekezaji ,prof  Adolf Mkenda ,imesema kuwa  hatua hiyo imekuja baada ya raisi  Magufuli kupata taarifa kuwa Mkurugenzi huyo alikua hachukui mshahara wa serikali tangu alipoajiriwa  mwaka 2013 hatua ambayo Rais amezua maswali mengi  Aidha taarifa hiyo iliyosainiwa na katibu mkuu huyo imeongeza kuwa endapo BI kairuki atakua tayari kuendelea kufanaya kazi nyingine huku mchakato wa kumpata  mkurugenzi mpya umeanza mara moja . kwa mujibu wa prof Mkenda bw clifford katondo tandali atakaimu nafasi ya mkurugenzi mtendaji wa kituo hicho cha uwekezaji nchini TIC.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni