C E O OF BMG

Picha yangu
FOUNDER AND OWNER OF BLACK GENERATION MEDIA GROUP, JORNALIST AND BROADCASTER BY PROFESIONAL.

Alhamisi, 26 Mei 2016

MABIGWA WA LIGI KUU NCHINI WINGEREZA LEICESTER CITY , WAKUBALI KUMWACHIA MSHAMBULIAJI WAO MMOJA KWA CLUB YA NCHINI UJERUMANI....

Mabigwa wapya wa soka Nchini  England Leicester City Wakubali kumuachia Mshambuliaji Aliyewasababishia  Gharama kubwa za usajili Mwanzoni mwa msimu huu .
Mabigwa hao wa soka nchini England, wamekubali kumuuza  Mshambuliaji  wao kutoka nchini croatia , ambaye aliwagharimu kiasi kikubwa cha pesa katika usajili wake mwanzoni mwa msimu huu, Andrej kramaric.
Leicester city wametoa baraka za kuondoka kwa kramaric, baada ya kukamilisha  mazungumzo ya biashara na uongozi wa klabu ya Hffenheim ya nchini ujerumani.
Kramaric alisajiliwa na The foxes mwaka 2015, akitokea kwenye klabu ya HNK Rijeka ya nchini Croatia kwa ada ya uhamisho wa  pauni millioni 9.7, lakini mwezi januari alipelekwa kwa mkopo nchini ujherumani katika klabu ya hoffenheim.
Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 24, ameuzwa kwa bei ya hasara ya pauni milioni 8, na amekubali kusaini mkataba wa miaka minne na klabu ya hoffenheim.
Kramaric, alilazimika kuondoka king power stadium wakati wa dirisha dogo la usajili, kufuatia kushindwa kupata nafasi ya kucheza kila mwishoni mwa juma, na kwake kutokana na uwezo wa washambuliaji wengine  klabuni hapo.
Uongozi wa Hffenheim, umefikia maamuzi ya kumsajili  moja kwa moja Kramaric, baada ya kuridhishwa na uwezo wake kisoka ambao ulisaidia kuinusuru klabu hiyo isishuke daraja msimu wa 2015-16.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni