C E O OF BMG

Picha yangu
FOUNDER AND OWNER OF BLACK GENERATION MEDIA GROUP, JORNALIST AND BROADCASTER BY PROFESIONAL.

Alhamisi, 28 Julai 2016

HATMA YA SAKATA LA KIUNGO PAUL POGBA KUTUA OLD TRAFORD KUJULIKANA NDANI YA SAA 48 ZIJAZO............

Sarakasi za usajili wa kiungo kutoka ufaransa [PAUL POGBA]hatma ya uhamisho wa mchezaji huyo kujulikana ndani ya saa 48.
Klabu hiyo ya manchester united yenye maskani yake katika jiji la Manchester nchini Wingereza inatarajia kukamilisha dili la kumsajili kiungo huyo kutoka Nchini Ufaransa na klabu ya Juventus ya nchini italia Paul pogba ndani ya saa 48 zijazo.
Man united wanatarajia kukamilisha dili hilo kwa ada ya uhamisho itakayovunja rekodi ya dunia, ambayo kwa sasa inashikwa na mshambuliaji kutoka Nchini wales na klabu ya Real madrid Gareth Bale.
Mashetani hao wekundu tayari wameshawasilisha ofa ya pauni milioni 100, huko Juventus stadium na baadhi ya vyombo vya habari vimeripoti kuwa uongozi wa mabigwa wa soka nchini Italia Juventus umeshakubali.
Jambo lingine ambalo linaonyesha dalili za dili la wa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 huenda likakamilishwa ndani ya saa 48 zijazo ni mazungumzo ya uhamisho huo kati ya wakala wa Pogba Mino Raiola, na Mkurugenzi wa club hiyo ya Juventus Giusppe Beppe Moratta.
Mwanzo wawili hao walikua wakipingana kuhusu swala la uhamisho wa mchezaji huyo.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni