C E O OF BMG

Picha yangu
FOUNDER AND OWNER OF BLACK GENERATION MEDIA GROUP, JORNALIST AND BROADCASTER BY PROFESIONAL.

Alhamisi, 28 Julai 2016

NEW HIT FROM KALA JEREMIAH FT MIRIUM CHIRWA WANANDOTO WATCH IT HERE............................

KOFFIE OLOMIDE ATUPWA JELA MIEZI 18 MJINI KINSHASA NCHINI CONGO............

Mahakama mjini kinshasa imemuhukumu mwanamuziki Mkogwe Koffie Olomide kwenda jela miezi 18 kwa kosa la kumpiga mngenguaji wake kudhalilisha utu wa mwanamke.
Hukumu hiyo ilitolewa juzi mjini humo imemtaja mkogwe huyo kama sugu wa makosa hayo ambayo amekua akiyatenda mara kadhaa
Msanii huyo ameanza kutumikia adhabu yake katika gereza moja nchini humo na wakati akiingia kwenye gereza hilo Koffie alisikika akisema siwapendi wanawake,

KLABU YA VILLARREAL YAKAMILISHA USAJILI WA MSHAMBULIAJI KUTOKA CHELSEA......................................

Klabu ya Villarreal ya nchini Hispania imedhibitisha kumsajili Mshambuliaji kutoka nchini Brazil ,Alexandre pato
Villarreal wamekamilisha usajili wa mshambuliaji huyo ambae mwanzoni mwa mwaka huu alisajiliwa kwa mkopo na klabu ya chelsea yanchini wingereza akitokea Corithians ya nchini Brazil.
Taarifa zilizochapishwa kwenye tovuti ya klabuhiyo ya El Madrigal zimeeleza kuwa pato amesaini mkataba wa miaka minne.
Hata hivyo haikuelezwa ni kiasi gani cha pesa kilichotumika kama ada ya usajili wa mshambuliji huyo mwenye umri wa miaka 26, ambaye aliwahi kutamab na klabu ya AC milani ya nchini italia kuanzia mwaka 2007-2012.
Klabu ya sevilla cf ya nchini Hispania nayo ilikua inahusishwa na kutaka kumsajili Pato.

HATMA YA SAKATA LA KIUNGO PAUL POGBA KUTUA OLD TRAFORD KUJULIKANA NDANI YA SAA 48 ZIJAZO............

Sarakasi za usajili wa kiungo kutoka ufaransa [PAUL POGBA]hatma ya uhamisho wa mchezaji huyo kujulikana ndani ya saa 48.
Klabu hiyo ya manchester united yenye maskani yake katika jiji la Manchester nchini Wingereza inatarajia kukamilisha dili la kumsajili kiungo huyo kutoka Nchini Ufaransa na klabu ya Juventus ya nchini italia Paul pogba ndani ya saa 48 zijazo.
Man united wanatarajia kukamilisha dili hilo kwa ada ya uhamisho itakayovunja rekodi ya dunia, ambayo kwa sasa inashikwa na mshambuliaji kutoka Nchini wales na klabu ya Real madrid Gareth Bale.
Mashetani hao wekundu tayari wameshawasilisha ofa ya pauni milioni 100, huko Juventus stadium na baadhi ya vyombo vya habari vimeripoti kuwa uongozi wa mabigwa wa soka nchini Italia Juventus umeshakubali.
Jambo lingine ambalo linaonyesha dalili za dili la wa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 23 huenda likakamilishwa ndani ya saa 48 zijazo ni mazungumzo ya uhamisho huo kati ya wakala wa Pogba Mino Raiola, na Mkurugenzi wa club hiyo ya Juventus Giusppe Beppe Moratta.
Mwanzo wawili hao walikua wakipingana kuhusu swala la uhamisho wa mchezaji huyo.

RAPA NAY WA MITEGO ADAI ATAWAMIS......

Rapa Nay wa mitego ambae amefungiwa kujihusisha na shuhuli za muziki na Baraza la sanaa nchini BaSATA, amefunguka na kudai kuwa atazimiss shuhuli alizokua anazifanya.
Kupitia ukurasa wake wa istagram, rapa huyo ameweka picha akiwa jukwaani na kuandika ujumbe uliosomeka "daa nitazimiss sana hizi.
Basata imemfungia rapa huyo kwa kipindi amabacho hakijajulikana, mpaka pale watakapojiridhisha kwamba amebadilika ikiwemo kujisajili kufanya shuhuli za sanaa nchini.

Jumatano, 13 Julai 2016

KLABU YA CHELSEA YAZINDUA RASMI JEZI ITAKAYOTUMIKA KATIKA MSIMU UJAO WA LIGI KWA MECHI ZA UGENINI...........

klabu ya chelsea yenye maskani yake jijini london nchini wingereza yazindua rasmi jezi itakayo tumika katika mechi zake za ugenini.
klabu hiyo amabyao kwa sasa inaongozwa na kocha mpya Antonio conte baada ya kutimuliwa kwa kocha wa awali Jose morinho ipo katika maandalizi ya kujiandaa na msimu ujao wa ligi kuu nchini wingereza, imezindua rasmi jezi hiyo itakayo tumika  katika mechi zake zote za ugenini kwa msimu ujao wa 2016-2017...

ITAZAME HAPA BRAND NEW JOINT FROM DIMOND PLATNUM FT P SQUARE KIDOGO OFFICIALY VIDEO......................

MAMA WA CRISTIANO RONALDO AMJIA JUU MCHEZAJI WA UFARANSA DIMITRI PAYET......................................

Mama wa Cristiano Ronaldo Dolores Aveiro amjia juu Dimitri payet,kufuatia rafu mbaya aliyomchezea mwanae katika fainali ya EURO 2016  Nchini Ufaransa.
Malalamiko hayo yametolewa na mama mzazi wa cristiano Ronaldo,baada ya mwanae kuumia katika fainali ya kombe la michuano ya mabara ya ulaya UEFA EURO, ambapo katika mchezo huo wa fainali uliwakutanisha Timu ya taifa ya ureno dhidi ya Ufaransa waliokua wenyeji wa michuaano hiyo, ambapo katika kipindi cha kwanza mchezaji huyo aliumia baada ya kuchezewa rafu mbaya na mchezaji wa ufaransa Dimitri payet hali iliyopelekea mchezaji huyo kushindwa kuendelea na mchezo,huyo na kutolewa nje ya uwanja huku akitokwa machozi, hali iliyopelekea mama mzazi wa mchezaji huyo kuja juu na kudai kua mchezaji huyo wa ufaransa Dimitri Payet alikusudia kumchezea mwanae rafu hiyo kwa kuandia katika ukurasa wake katika mtandao wa twiter  ''to play football is to kick a ball and not to kick the legs,,aliandika mama huyo.
Hata hivyo mechi hiyo iliisha kwa timu ya Taifa ya Ureno kufanikiwa kutwaa ubigwa wa michuano hiyo kwa kufanikiwa kuifunga Ufaransa goli  moja kwa sifuri goli lililofugwa na mchezaji Heder katika dakika 30 za nyongeza baada ya kukamilika dakika 90 za kawaida bila mshindi kupatikana.

THIERY HENRY AAMUA KUACHANA NA KAZI YA UKOCHA KATIKA CLUB YA ARSENAL.......................................

Gazeti la The sun linaripoti kuwa Thiery Henry ameachanana kazi ya ukocha wa muda wa timu ya vijana ya Arsenal baada ya kupishana kauli na meneja Arsener Wenger kufuatia kazi yake ya uchambuzi wa masuala ya soka kwenye Television.
Thiery Henry alikua anafanya kazi kwa part time na Arsenal ,kama kocha wa vijana chini ya umri wa miaka 18,alipata leseni ya UEFA  wakati huohuo akiwa ni mchambuzi wa kituo cha Television cha Sky sport, Henry aliomba kupewa mkataba wa kufanya kazi na Arsenal kwa msimu unaokuja kwa malipo kidogo, lakini boss wake Arsenel wenger alimpa mashsrti ya kufanya kazi hiyo kwa kumwambia kama anataka kazi hiyo basi aachane na kazi ya sky sports na kama anataka kazi Sky sport basi aachane na Arsenal.
Maamuzi aliyofanya Henry ambae ni gwiji wa soka wa zamani wa club hiyo yenye maskani yake katika jiji la London nchini wingereza, ameamua kuacha kazi katika Club hiyo na kubaki kuwa mchambuzi katika kituo cha Television cha Sky sport.
Maamuzi hayo yaliyofanywa na Gwiji huyo yamewafurahisha baadhi ya viongozi wa club hiyo ya Arsenal..

Ijumaa, 8 Julai 2016

MAMIA YA WATU WATAPIGWA PICHA ZA UTUPU KATIKA MJI WA HULL NCHINI UINGEREZA.........................

Mamia ya watu watavua nguo zao na kupigwa picha wakiwa tupu kusherekea utamaduni katika mji wa Hull, uingereza.
Tukio hilo litakuwa la kusherekea mji huo kama mji wa utamaduni.
washiriki watapakwa rangi ya samawati jumamosi na kisha wapigwe picha wakiwa katika maeneo mashuhuri jijini humo kama sehemu ya mradi uliopewa jina Sea of Hull.
Mradi huo unatekelezwa nampiga picha spencer Tunick na unadhaminiwa na taasisi ya sanaaa ya Ferens Art Gallery.
picha zitakazopigwa zitawekwa na kuoneshwa kwa umma wakati wa tamasha ya sanaa ya 2017 itakayoendelea kwa mwaka mmoja.
Tunick, anayetoka New York, amewahi kufanya kazi kama hiyo kwingine.
 Amewahi kupiga picha za watu wengi wakiwa uchi sydney opera House, place des Art mjini Montrel, Mexico city na mjini Munich nchini  Ujerumani.
Bw Tunick amesema kazi zake'' hugusia historia ndefu ya sanaaa ya utupu''
''Mavazi ni sanaa ya mtu mwingine''anasema.
Fashion ni sanaa. kwa kuondoa hilo[ mavazi] nitakuwa nafanya kazi na usawa na maumbile katika umaridadi wake''
Watu karibu 2000 wamejiandikisha kupigwa picha tangu wazo hilo litangazwe mwezi machi.
Baraza la mji wa Hull limesema baadhi ya barabara zitafungwa wakati wa shuhuli hiyo jumamosi asubuhi.

PAUL POGBA AKIRI KUA ANAHITAJI KURUDI KATIKA CLUB YA MANCHESTER UNITED.......

Jarida maarufu huko nchini ufaransa L ,Eguipe limedai  kiungo wa Juventus na timu ya taifa ya Ufaransa Paul pogba amewaambia marafiki zake na wachezaji wenzake kwamba anataka kurejea Man United ikiwa ni Miaka minne tangu aondoke Old Trafford kwenda kujiunga na klabu ya Italy Juventus.

Jumatatu, 4 Julai 2016

MABASI MAWILI YA CITY BOYS YAUWA 24 MKOANI SINGIDA...

Mabasi ya  City boys yanayofanya safari zake kutoka dar es salam ,mwanza,na Shinyanga Dar es salam, yamepata ajali katika eneo la Miwani mkoani Singida na watu 24, wamepoteza maisha papo hapo na wengine wamejeruhiwa vibaya,baada ya kugongana uso kwa uso..

MANCHESTER UNITED WAPO TAYARI KULIPA PAUNDI MILIONI100 KWA JUVENTUS............

Manchester united wamewaambia juventus kuwa wako tayari kulipa pauni million 100 kumsajili kiungo kutoka ufaransa paul pogba 23,na watampa mshahara wa pauni 250,000 kwa wiki.

HAYA NDIO MANENO ALIYOYASEMA BARAKA THE PRINCE, KUMUHUSU MSANII MWENZAKE YOUNG KILLA.

Msanii Baraka the prince, amesema kua hajawai kuzipenda nyimbo za msanni mwenzake Young killa, na wala hategemei kuzipenda nyimbo za msanii huyo mwenzake,
MSanii huyo ametoa maneno hayo wakati akiwa anafanya mahojiano na kituo kimoja cha redio
Hata hivyo kauli hiyo imeonekana kupokewa katika mtazamo tofauti na mashabiki wa mziki wa kizazi kipya, wengi wameonekana kumponda msanii huyo kwa kauli hiyo aliyoitoa na kusema, young kila ni msanii mkubwa na mwenye kipaji cha aina yake, hivyo Baraka the prince bado ni msanii mchanga sana  katika tasnia ya mziki wa kizazi kipya hivyo hawezi kushindana na young killa.