C E O OF BMG

Picha yangu
FOUNDER AND OWNER OF BLACK GENERATION MEDIA GROUP, JORNALIST AND BROADCASTER BY PROFESIONAL.

Jumatano, 29 Juni 2016

CLUB YA CHELSEA IPO KATIKA HATUA ZA MWISHO KUKAMILISHA USAJILI WA MSHAMBULIAJI KUTOKA OLYMPIC MARSEILLE YA NCHINI UFARANSA

Club ya Chelsea yenye maskani yake jijini london nchini Wingereza ipo katika hatua za mwisho kumsajili Mshambuliaji kutoka club ya Olmpic Marseille, Batshuayi kwa ada ya Euro  million 33.
Mshambuliaji huyo ambae ni raia wa Ubelgiji anatarajia kujiunga na hiyo ya chelsea akitokea katika club ya olmpic Marseille ya nchini ufaransa,msimu uliopita mchezaji huyo alifanikiwa kuifungia club hiyo magoli 24 katika ligi ya nchi hiyo maarufu kama League one,.
Mchezaji huyo anatarajia kujiunga na mbelgiji mwenzake Eden hazard katika klabu hiyo ya chelsea katika msimu ujao.
Usajili huo ni wa kwanza kufanywa na club ya chelsea kwa msimu huu chini ya kocha mpya Antonio Conte, ikiwa ni moja ya harakati za kukiboresha kikosi cha club hiyo, kwani msimu uliopita haukua mzuri sana kwa club hiyo, iliyokua ikifundishwa na kocha  jose morinho aliyetimuliwa klabuni hapo baada ya club hiyo kupata matokeo mabaya, kitu kilichopelekea kumaliza katika nafasi ya tisa katika msimamo wa ligi kuu nchini wingereza na kukosa nafasi ya kushiriki michuano ya klabui bigwa barani ulaya katika msimu ujao.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni