C E O OF BMG

- Black generation media Group [ BMG]
- FOUNDER AND OWNER OF BLACK GENERATION MEDIA GROUP, JORNALIST AND BROADCASTER BY PROFESIONAL.
Jumanne, 29 Machi 2016
Ijumaa, 25 Machi 2016
Jumamosi, 19 Machi 2016
Alhamisi, 17 Machi 2016
Utata wa Filamu ya Lulu Michael Iliyoshinda Tuzo Nigeria..Wizara Yatoa Tamko Hili Hapa....

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Kumekuwa
na minongono mingi kutoka kwa baadhi ya wananchi kuhusu Filamu ya
Mapenzi ya Mungu ya msanii Elizabeth Michael (Lulu) iliyoshinda tuzo ya
Filamu bora Afrika Mashariki mapema mwezi huu huko Lagos Nchini Nigeria
katika tuzo za African Magic Views Choice Award (AMVCA).Ili filamu ikamilike inahusisha watu mbalimbali wanaoshirikishwa kukamilisha filamu kuanzia mtoa wazo ambaye wazo hilo huwekwa katika mswada na mtaalamu jambo ambalo haliondoshi umiliki wa filamu.
Tunapenda kuufahamisha umma kuwa mmiliki halali wa Filamu ya Mapenzi ya Mungu ni Msanii Elizabeth Michael (Lulu) na ndiye aliyepata tuzo kwani ana haki zote za kupata tuzo hiyo kama mmiliki halali wa filamu hiyo.
Filamu ya Mapenzi ya Mungu imetengenezwa chini ya kampuni ya Proin Promotion na imesajiliwa kwa namba ya usajili CO831190.
IMETOLEWA NA
WIZARA YA HABARI, UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO
Kama Wewe ni Msichana na Unamzidi Ruby Kuimba Njoo WASAFI Records - Babu Tale

Meneja wa lebel ya WCB Babu Tale ametoa
fursa kwa wasanii wa kike wenye vipaji kuonyesha vipaji vyao, na
hatimaye kuweza kupata fursa ya kuwa chini ya uongozi wao wa WCB.
Babu Tale ametoa fursa hiyo alipokuwa
akiongea ndani ya Planet Bongo ya East Africa Radio, alipoenda
kumtambulisha msanii mpya amabye atakuwa chini ya uongozi huo Raymond
TipTop, na kusema kuwa wasani wa kike ni wachche hivyo wana fursa kubwa
ya kufanya vizuri iwapo watajituma.
Tuna Plan kuwapata wasanii wa kike
lakini wenye vipaji vya ukweli, asikwambie mtu industry yetu ina
wanawake wachache, tungepata wananwake wanne hata watano', alisema Babu
Tale
Pia babu Tale alisema anatamani sana
msanii Ruby angekuwa kwenye management yake, kwani ana uwezo mkubwa
lakini kwa bahati mbaya ytayari yuko chini ya management nyingine ya
THT.
Kwangu mimi ingekuwa Ruby hayuko chini
ya THT, au hana management tungemchukua, lakini nasema hivi, kama
anakuja mwanamke, awe na level ya kufanana na Ruby au kumshinda Ruby",
alisema Babu Tale
Pamoja na hayo nae Diamond Platnums
amesema ameweka wazi vigezo ambavyo msanii huyo wa kike avifikie ili
aweze kuwa chini ya uongozi huo, pamoja na kujituma tofauti na
walivyozoea kuwa hawawezi.
Aweze kuandika mashairi, aandike nyimbo
zake mwenyewe unajua kuna kitu kimoja, wanawake washajiwekea kuwa wao
hawawezi, sio kweli hawataki kufocus na kujaribu", alisema Diamond.
Jumatano, 16 Machi 2016
Jumamosi, 12 Machi 2016
Jumatano, 9 Machi 2016
Jumanne, 8 Machi 2016
Jumatatu, 7 Machi 2016
Jisajili kwenye:
Machapisho (Atom)